Loading...

BAADA YA UKIMYA TANGU SUKARI KUTOKA NJE KUZUIWA, BEI MPYA YA SUKARI YATANGAZWA RASMI.....

TUFUATE INSTA KWA KUBONYEZA HAPA



HATIMAYE  Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli  imekisikia kilio cha muda mrefu  cha Wananchi ambao  walikuwa wakilalamika kupanda  kwa  bei ya sukari nchini. 

..sifa 10 za mpenzi mwaminifu 

.TB Joshua aonyesha maajabu

Akizungumza na Waandishi wa Habari  mchana huu  jijini Dar es Salaam Mkurugenzi  mkuu wa Bodi ya Sukari nchini Tanzania, Henry Semwaza amesema kuanzia sasa kilo moja ya  sukari itauzwa sh.  1800 nchi nzima. 

"Serikali, kupitia bodi ya Sukari Tanzania, inawaarifu wananchi wote kuwa bei ya rejareja ya sukari sasa itakuwa sh. 1,800 kwa kilo moja
. "Amesema Semwaza na kuongeza;

" Wafanyabiashara wote wanapaswa kuzingatia agizo hili, pamoja na kuhakikisha kuwa sukari inaendelea kusambazwa na kuuzwa kwa wananchi bila kuihodhi.

Maafisa biashara wa mikoa na wilaya watafuatilia na kusimamia utekelezaji wa agizo kuhusu bei elekezi ya sukari, na hawatasita kuchukua hatua stahiki za kisheria kwa wale wote watakaobainika kupandisha bei ya bidhaa hiyo.




TUFUATILIE FACEBOOK KWA KUBONYEZA 'LIKE' HAPA CHINI.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by BoazMwakasege

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright UHONDO WA MTAA | Modified By PB Web and Graphics
Back To Top